Profesa Ndakidemi aipa Milioni tano familia iliyopoteza watu wanne kwenye mafuriko Kata ya Kimochi

 


Profesa Ndakidemi aipa Milioni 5 familia iliyopoteza watu wanne kwenye mafuriko Kata ya Kimochi

 Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini (ccm),Profesa Patrick Ndakidemi ametimiza ahadi yake baada ya kuipa shilingi Milioni tano familia iliyopoteza watu wanne ambao walifari Dunia baada ya nyumba yao kuangukiwa na kifusi baada ya mvua kubwa Iliyonyesha usiku wa April 25 Mwaka huu .

Mvua hiyo ambayo ilileta uharibifu mkubwa Katika maeneo mbali mbali ya mkoa wa Kilimanjaro ilisababisha mafuriko ambayo yaliharibu Mali za watu zikiwamo nyumba ,mifugo,vyakula.

Profesa Ndakidemi alitoa ahadi hiyo wakati wa mazishi ya watu hao Katika kata ya Kimochi jimboni humo.

Alisema kiasi hicho cha fedha kitatumika kuwarejeshea makazi yao baada ya nyumba Yao kuanguka na kukosa makazi.

Katika mazishi hayo,Profesa Ndakidemi alitoa ubani wa shilingi laki tano kwa familia hiyo huku akitoa tani mbili za mahidi kwa wananchi wa Kata za Mabogini na Arusha chini ambazo ziliathiriwa na mafuriko hayo.

Mwenyekiti wa ukoo wa Mchaki,Elikunda Chaki amesema profesa Ndakidemi alitimiza ahadi yake Agosti 21 mwaka huu kupitia kwa Katibu wake,Alois Robert.

"Ni kweli mheshimiwa mbunge alimiza ahadi yake na sisi kama familia tumemshukuru kwa kukamilisha ahadi yake",amesema Chaki.

Septemba 11 mwaka huu familia hiyo ya Chaki ikamwandilia barua ya shukrani Profesa Ndakidemi kutokana na kutimiza ahadi yake.

"Mhe.Mbunge wa Moshi Vijijini husika na mada tajwa hapo juu,sisi wanafamilia wa familia hizi mbili tunapenda kuleta shukrani za kipekee kwa kwa mchango wako uliowezesha ujenzi wa nyumba kwa ndugu zetu katika maafa ya mafuriko katika kata ya Kimochi ,kijiji cha Lyakombilo".

Familia hiyo ikahitimisha salama za pongezi kwa mbunge huyo kwa kunukuu maandiko matakatifu kutoka kitabu cha Mathayo sura ya 25 mstari wa 40 na hapa nanukuu

"Na mfalme akajibu,akawaambia Amin nawaambia kadri mlivyomtendea mmojawapo na hao ndugu zangu waliowadogo,mlinitendea mimi ".mwisho wa kunukuu.

Zaidi ya watu 4,000 wariripotiwa kuathiriwa na mafuriko hayo yaliyosabishwa na mvua kubwa zilizokuwa zikiendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Kilimanjaro.

Mbali na hao zaidi ya Kaya 906 ziriripotiwa kuathiriwa na mafuriko hayo huku watu sita wakiripotiwa kufariki dunia kutokana na mvua hizo.

 

Post a Comment

0 Comments