KIBOSHO MAGHARIBI -MOSHI
WANANCHI wa
kata ya Kibosho Magharibi wametuma salamu kwa madiwani na wabunge wawili
wanaounda halmashauri ya wilaya ya Moshi(Moshi DC)wakipendekeza Diwani mteule
anayesubiria kuapishwa kuwa Diwani wa kata hiyo Deo Mushi apeperushe bendera ya
mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo.
Halmashauri
ya wilaya ya Moshi inaundwa na majimbo mawili ya uchaguzi ambayo ni Vunjo na
Moshi Vijijini na katika Baraza la madiwani lililopita mwenyekiti wa
halmashauri hiyo alikuwa Morris Makoi akitokea kata ya Okaoni na sasa anagombea
kiti cha Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha mapinduzi(CCM)jimbo la Moshi Vijijini.
Upatu huo wa
kumtaka Deo Mushi awe mwenyekiti wa halmashauri hiyo ulianza kupigwa kitambo na
juzi juzi wakati wa mkutano wa Kampeni za udiwani katika Kijiji cha Manushi
Ndoo,mwananchi mmoja alinyoosha mkono akiomba kuzungumza na alipopewa kipaza
sauti alianza kumwagia sifa kada huyo wa CCM akidai anauzoefu wa kutosha
kuweza kushika nafasi hiyo.
“Nakuomba
sana mheshimiwa Morris Makoi ile nafasi yako ya mwenyekiti wa halmashauri ya
wilaya umwachie kaka yetu Deo Mushi,tunamwamini anauzoefu mkubwa wa kuongoza
halmashauri hiyo,tunakuomba sana”,alisema mama huyo Agustina Faustine Munishi huku
akishangiliwa na umati mkubwa wa wananchi waliojiotokeza katika mkutano huo.
Joto la
kuwania nafasi hiyo ya mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Moshi linazidi
kupanda kila uchao hata kabla ya uchaguzi mkuu wa Rais,wabunge na madiwani
utakaofanyika jumatano ya Oktoba 29 ambako madiwani wanaotoka upande wa jimbo
la Vunjo nako moto ukiwaka wa nani apeperushe bendera hiyo kutokea upande huo.
Kwenye
mkutano huo wananchi walipewa nafasi ya kuzungumzia kero zao katika kata hiyo
na baadhi yao wakatoa kilio chao juu ya uhaba wa walimu katika baadhi ya shule
zao za msingi hatua ambayo imewafanya kutoa fedha mara kwa mara kwa ajili ya
kulipia malipo ya walimu wa kujitolea..
Kilio
kingine cha wananchi wa kata hiyo ni kupewa Ankara kubwa za maji ambazo
haziendani na uhalisia wa matumizi ya maji hoja iliyoungwa mkono na mgombea
huyo wa kiti cha udiwani na kuahidi kushughulikia kero hiyo mara tu
atakachaguliwa kuwa diwani wa kata hiyo.
Akizungumza
na wananchi katika mkutano huo wa kampeni,Deo Mushi alisema Ankara za maji
zimekuwa kero kubwa kwa wananhi wa kata hiyo na ameahidi kushuhulikia kero hiyo
ambayo imekuwa ni ya muda mrefu kwa wananchi hao.
Aliwataka wananchi wa kata hiyo kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kuwaomba kumpigia kura nyingi mgombea wa kiti cha urais kupitia Chama cha mapidunzi(CCM),Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan,mgombea kiti cha ubunge jimbo hilo,Morris Makio nay eye mwenyewe ili kujenga utatu mtakatifu au mafiga matatu,






0 Comments