K’NJARO TUPO TAYARI KWA UCHANGUZI MKUU,ASEMA RC NURDIN BABU,AONYA WANAOJIPANGA KULETA VURUGU

 

   Nurdin Babu,mkuu wa mkoa wa Kilimanajro
 

KILIMANJARO-TANZANIA

SERIKALI  imewahikikishia wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro kuwa uchaguzi mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu utafanyika ktika hali ya amani na utulivu wa hali ya juu kwa aslimia mia moja na kuwaonya wote wanaojiandaa kuvuruga uchaguzi huo kuwa watakabiliwa na mkono wa dola.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 19,2025 ofisini kwake,Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Nurdin Hassan Babu amesema hadi sasa hali ya usalama katika mkoa wake ni shwari na wananchi wapo tayari kwa uchaguzi mkuu.

Alitoa wito kwa wananchi wote waliojiandikisha kupiga kura kutumia haki yao ya kikatiba  kujitokeza kwenda kupiga kura bila hofu na bila woga wowote na kwamba mara baada ya kupiga kura waendelee na shughuli zao kwani matokeo ya kura yatabandikwa kwenye mbao za matangazo.

“Tumewaita tuwape taarifa kwamba,wananchi ifikapo terehe 29 mwezi wa kumi siku kumi kuanzia leo wananchi wote waliojiandikisha kupiga kura waende kwenye vituo bila wasiwasi na bila hofu yoyote”,alisema.

“Sasa yapo mambo mengi ya mitandaoni ,wananchi hayo naomba  wayaache,mimi kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama nawahakikisha usalama kwa aslimia mia moja,baada ya kupiga kura kila mwanachi aende kwenye shughuli zake za kujiletea maendeleo”

“Kama kuna mtu amejipanga vizuri na ana misuri mikubwa tutamuona huko mbele,ninachoweza kuwahakikisha wananchi wa mkoa wa kilimanajro uchaguzi huu kwa mkoa wa kilimanjaro utafanyika katika hali ya utulivu na haijawahi kutokea”,amesema.

Kumekuwepo na taarifa za watu kupitia mitandao ya kijamii kutishia kuandamana kwa lengo la kuvuruga mchakato mzima wa zoezi la upigaji kura kwa maslahi yao binafsi kitendo ambacho serikali na vyombo vya ulinzi na usalama vimeendelea kuonya kuwa haitowavumilia watu wa aina hiyo.

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania(TCRA)kwa upande wake imekuwa ikitoa wito kwa watanzania na watumiaji wa mitandao ya kijamii kutumia mitandao hiyo vizuri na kuacha kuitumia kwa misingi isiyokuwa sahihi.



Vyama mbali mbali vya siasa nchini vipo katika kampeni za kunadi sera kwa wananchi kuomba ridhaa ya kuchaguliwa hapo oktoba 29 kampeni ambazo zilianza septemba 28 mwaka huu na zitahitimishwa Oktoba 28 mwaka huu na siku inayofuata Taifa litakuwa linaingia kwenye uchaguzi mkuu.

Viongozi mbali mbali wa dini na makundi mengine ya kijamii wameendelea kuwataka watanzania kuendelea kuenzi na kudumisha  amani iliyoachwa na waasisi wa taifa hili akiwamo Baba wa Taifa Hayati Mwlimu Julius Nyerere.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Nurdin Babu akiwa na wajumbe wa kamati ya Ulinzi na usalama ya mkoa wakati wamkutano wake na waandishi wa habari ofisini kwake leo Oktoba 19,2025

Post a Comment

0 Comments