JESHI la polisi mkoa wa Mbeya linamshikilia mtanzania mmoja Stanslaus Mazengo(51)mkazi wa Isitu mkoani humo akituhumiwa kusafrisha wahamiaji haramu 38 raia wa Ethiopia kwa kutumia gari lake dogo aina ya Toyota Noah lenye namba sa usajili T953DJF.
kwa mujibu
wa taarifa ya jeshi la polisi mkoani Mbeya,wahamiaji hao haramu walikamatwa
Novemba 11 mwaka huu katika pori la Lanchi ya Matebele lililopo katika kijiji
cha Igumbilo mkoani Mbeya.
Kulingana na
taarifa ya kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Kamishina Msaidizi mwandamizi wa
polisi(SACP),Benjamin Kuzaga ,baada ya mahojiano dereva huyo alidai kuwa
alikuwa akiwapeleka watuhumiwa hao kwenda kuwahifadhi kwenye nyumba ya Mwanamke
mmoja(jina tunalihifadhi)katika eneo la Chimala.
Kulingana na
taarifa ya jeshi la polisi,wahamiaji hao haramu walikuwa wasafrishwe kwa njia
za panya na kuvuka mpaka wa Tanzania kwenda nchini Afrika kusini.
Mtandao wa
kusafrisha wahamiaji haramu umekuwa ukihusisha watanzania wakishirikiana na
raia wa nchi jirani ambako inadaiwa wamekuwa wakijiingizia fedha nyingi kupitia
biashara hiyo haramu,
Hata
hivyo,jeshi la polisi mkoani Mbeya limetoa rai kwa wananchi wenye tamaa ya kujipatia fedha kuacha
tabia ya kuwawezesha raia wa kigeni kuingia ama kupita nchini bila kufuata
taratibu za kisheria na badala yake wawaelekeze kufuata taratibu kupitia mamlaka
husika ili kuepuka usumbufu ikiwamo kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria
.




0 Comments