DKT. NGWARU MAGHEMBE AZINDUA KAMPENI NA KUAHIDI KUPAMBANA NA TATIZO LA TEMBO WILAYANI MWANGA MAJI, ELIMU, AFYA, UMEME NA MIUONDOMBINU YA BARABARA NI MOJA YA VIPAUMBELE VYAKE KWA WANANCHI


MWANGA-KILIMANAJRO

MGOMBEA ubunge jimbo la Mwanga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM),Dkt.Ngwaru Jumanne Maghembe, amezindua rasmi kampeni za ubunge na kuahidi kushughulikia kero kubwa zinazowakabili wananchi wa jimbo la Mwanga ikiwamo tatizo kubwa la uvamizi wa Tembo ambao wamekuwa tishio kwa usalama na mali za wananchi hao.

Dkt.Ngwaru ambaye aliteuliwa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa baada ya kupata ushindi mkubwa kwenye kura za maoni wa kura 4,108 akimbwaga aliyekuwa mbunge wa Jimbo hilo,Wakili Joseph Tadhayo aliyeambulia kura 1,689,alizindua kampeni zake kwenye Tarafa ya Usangi.

Katika uinduzi huo,Dkt.Ngwaru alisema atashirikiana na TAWA kuhakikisha k inajengwa kituo cha kukabiliana na Tembo eneo la Jipendea ambako ni moja ya maeneo ambayo yamekuwa yakikabiliwa na uvamizi wa tembo kwenye makazi ya watu pamoja na kuharibu mazao yao.

“Tutahakikisha tuna fungua ofisi pale Jipendea ili wenzetu wa Tarafa ya Jipendea, Kwakoa, Mgagao, Toroha  na Kirya wasiendelee kupata shida na hili tutashirikiana na wenzetu wa TAWA ili tuwe na ofisi Jipendea yenye vifaa vyote vya kukabiliana na tembo pamoja na askari wa kutosha“,alisema.

Kuhusu tatizo la maji katika baadhi ya maeneo jimboni humo,Dkt.Ngwaru aliahidi yeye kwa kushirikina na madiwani watakaochaguliwa kushughulikia kero hiyo ya maji ambayo imkuwa ni ya muda mrefu.

Alipongeza hatua ya serikali kuufufua mradi mkubwa wa maji wa Mwanga-Same-Korogwe ambao ulikuwa ni wa kusuasua hadi hapo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipoamua kutoa pesa kuuendeleza.

“Mimi nimekuwa  mbunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki  kwa miaka minane, nchi yetu ni tofauti kabisa na nchi  nyingine ndani ya Jumuiya,ni bahati nzuri sana sisi tunaishi kwa Amani na Uhuru pamoja na mipango mizuri ya kuwaletea maendeleo wananchi”alisema na kuongeza.

“Hii ni kutokana na kuwa na viognozi wachapa kazi na makini chini ya Jemedali wetu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais ni mfuatliaji mzuri wa miradi ya maendeleo ukiwamo mradi wa maji wa Mwanga-Same hadi Korogwe.”

“Mradi huu ulioanza mwaka 2014 ulisuasua sana hadi Rais wetu alipoamua kutoa pesa ili mradi uendelee na sasa mradi huo umekamilika haya yote ni kwa sababu ya kuwa na viongozi wachapa kazi”,alisema.

Kwenye suala la Afya, Dk.Ngwaru alisema atahakikisha vituo vyote vya afya pamoja na zahanati vinajengwa  ili kuwaondoea kero wananchi wa jimbo la Mwanga na kuahidi kutoa fotari 5,000 na mifuko 100 ya saruji kwa kila zanahati itakayojengwa.

Alisema hadi sasa serikali imeweza kujenga majengo 10 kwenye Hospital  mpya ya Wilaya ya Mwanga na kwa sasa bado majengo 18 yatajengwa ikiwamo chumba cha upasuaji pamoja na ujenzi wa kituo cha Afya Chomvu kitakachokuwa na jengo la huduma ya  mama na mtoto.

Akizungumzia changamoto ya miundombinu ya barabara alisema mpango wa serikali ni kujenga barabara kwa kiwango cha lami kwa baadhi ya barabara ambazo ni mhimu katika shughuli za uzalishaji mali.

Aliahidi pia ujenzi na ukarabati wa minada ya ng’ombe ya Kileo na Mgagao lengo ni kuifanya minada hiyo kuwa kitovu kikubwa kwa Kanda wa kaskazini huku akiahidi kushughulikia suala la umeme kwenye vitongoji sita ambavyo havina umeme.

Dkt.Ngwaru aliahidi kushughulikia ukarabati na uboreshaji wa miundombinu ya umwagiliaji ikiwamo ujenzi wa soko la mazao la Kituli.






Post a Comment

0 Comments