MWANGA-KILIMANJARO
MBUNGE wa Bunge la
Jumuiya ya Afrika Mashariki na mgombea ubunge jimbo la mwanga kwa tiketi ya
Chama cha mapinduzi(CCM),DKT.Gwaru Jumanne Maghembe,ameahidi kuendeleza pale walipoishia
watangulizi wake.
Dkt.Gwaru ametoa kauli
hiyo wilayani mwanga mkoani Kilimanjaro muda mfupi baada ya kuchukua fomu ya
uteuzi kuwania kiti cha ubunge kwenye jimbo hilo kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi
jimbo la mwanga.
Alianza kumshukuru waziri
Mkuu mstaafu na Baba wa Mwanga,marehemu Cleopa David Msuya ambaye alikuwa
mbunge wa kwanza wa jimbo la mwanga.
Pili akamshukuru Profesa
Jumanne Maghembe ambaye pia ni Baba yake mzazi aliyehudumu katika jimbo hilo
kwa muda wa miaka 25.
Dkt.Ngwaru pia
alimshukuru mtangulizi wake wakili Msomi Joseph Thadayo na kueleza kuwa
atashughulikia changamoto ya umeme kwa baadhi ya vijiji ambavyo havina nishati
ya umeme ndani ya jimbo hilo.
Pia aliahidi kushughulikia changamoto ya ukosefu wa vyumba vya Madarasa kwa baadhi ya shule za msingi
jimboni humo.
Akizungumza na umati wa wanachama wa chama hicho waliofulika nje ya jengo jipya la Halmashauri ya wilaya ya Mwanga, Dkt.Ngwaru alisema uchaguzi ndani ya chama umemalizika na sasa nguvu inaelekezwa katika kuhakikisha jimbo hilo linabaki mikononi mwa CCM kwa chama hicho kupata ushindi wa kishindo.
Kwenye kura za maoni ndani
ya chama hicho,Dk. Ngwaru Jumanne Maghembe aliibuka mshindi kwa kupata kura 4,108 huku akimuacha kwa mbali mshindnani wake
na aliekuwa mbunge wa jimbo hilo Joseph Anania Thadayo,aliyepata kura 1,689, huku
ndugu Ramadhani Ally Mahuna akifuatia kwa kupata kura 720.






0 Comments