Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Nurdin Hassaan Babu,akizungumza kwenye uzinduzi wa Tamasha la Sita la kuhamasisha unywaji wa kahawa
MOSHI-KILIMANJARO
MKUU wa Mkoa wa
Kilimanjaro,Nurdin Hassan Babu,amezindua Tamasha la sita la uhamasishaji wa
unywaji wa kahawa na kupiga marufuku ukataji ovyo wa mibuni iliyozeeka.
Marufuku hiyo ameitoa mjini moshi wakazi akizundua Tamasha hilo tukio
lililofanyika makao makuu ya Bodi ya kahawa Tanzania(TBC)mjini Moshi na
kuhudhuliwa na wadau mbalimbali wa kahawa wakiwamo wakulima.
Wadau wengine walioshiriki tamasha hili ni pamoja na wanunuzi
wa kahawa wa ndani nan je ,wakaagaji wa kahawa,wakoboaji wa kahawa kwa maana
wenye viwanda vya kukoboa kahawa na wengineo.
Amesema mkoa wa Kilimanjaro unabebwa na zao la kahawa ukiachilia
mbali mazao mengine kama ndizi na mahindi hivyo akawataka wananchi wa mkoa huo
kulienzi zao hilo.
Alitoa wito kwa wakulima kung’oa mibuni ya zamani iliyozeeka na kupanda miche bora ya kahawa isiyoshambuliwa na wadudu na si kukata mibuni hiyo na kupanda mazao mengine,
Aliwaasa wakulima kuwatumia wataalamu wa kilimo wakiwamo maofisa
ugani watakaowapa elimu juu ya kupanda miche bora na kuwaasa vijana kujikita kwenye
kilimo cha kahawa badala ya kukaa vijiweni.
Mkuu huyo wa mkoa amesema kahawa ya Kilimanjaro inao muonjo
mzuri na imekuwa ikipendwa na watu wengi dunia hivyo aksisitiza umhimu wa
kuitunza kwani kwa sasa bei ya kahawa ipo juu tofauti na miaka ya hivi
karibuni.
Mwenyekiti wa Tamasha hilo,Denis Mahulu anasema lengo la kuandaa
tamasha hilo ni katika jitihada za kuongeza soko la ndani la unywaji wa kahawa
ambao kwa sasa upo aslimia saba tu huku aslimia 93 ya kahawa yote inayozalishwa
Tanzania ikiuzwa nje ya nchi.
Takwimu zinaonyesha kuwa ,unywaji
wa kahawa duniani unatarajia kuongezeka msimu ujao hadi kufikia magunia milioni
179 huku Ulaya,Marekani na Brazil zikiongoza kwa aslimia 2.25 ya unywaji.
Wakati hali ya unywaji wa kahawa duniani ikitarajia
kuongezeka.,Tanzania bado inapambana kuona soko la ndani linaongezeka hadi
kufikia aslimia 15 miaka kumi ijao.
Mkurugenzi wa Bodi ya kahawa nchini(TCB)anabainisha kuwa licha
ya Tanzania kuwa nchi pekee yenye viwanda vya kuongeza thamani hadi
kupata kahawa ya mezani,bado unywaji wa kahawa upo chini kwa wastani wa aslimia
tano hadi saba.
Mikakati inayowekwa na Bodi hiyo kufikia kiwango hicho ni pamoja
na kuwa na soko la uhakika,kupunguza utegemezi wa masoko ya nje,kuongeza ajira
kwa wananchi na kuongeza thamani ya zao la kahawa.
Mkurugenzi wa Bodi ya Kahawa Tanzania(TCB),Primus Kimaryo akizungumza katika uzinduzi wa Tamasha la sita la uhamasishaji unywaji wa kahawa
0 Comments