Mjumbe wa kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Kilimanjaro,Adam Best Simba(kushoto)akinadi mgombea wa kiti cha Udiwani kata ya Bondeni Mnaispaa ya moshi,Haji Fundi Haji wakti wa mkutano wa kampeni uliofanyika kata ya Bondeni.
MOSHI-KILIMANJARO.
MJUMBE wa kamati
ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Kilimanjaro na mratibu wa kampeni
wa CCM mkoa ,Adam Best Simba amewataka wananchi wa jimbo la Moshi mjini na mkoa
wa Kilimanjaro kwa ujumla kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura katika
uchaguzi mkuu oktoba 29 mwaka huu ili kukipa ushindi chama hicho.
Best Simba
alitoa wito huo kwenye mkutano wa kampeni za chama hicho Jimbo la Moshi mjini
zilizofanyika kwenye kata ya Bondeni Manispaa ya Moshi ambako alitumia mkutano
huo kumnadi mgombea wa kiti cha ubunge Ibrahim Shayo na mgombea udiwani Kata ya
Bondeni,Haji Fundi Haji.
Akizungumza
katika mkutano huo kada huyo wa CCM na mfanyabiashara maarufu nchini,alisema
hana shaka na ushindi wa Chama Cha Mapinduzi hapo oktoba 29 mwaka huu kuanzia
nafasi ya Rais,Ubunge hadi kwa madiwani na kuwataka wananchi kujitokeza kwa
wingi kupiga kura.
“Naomba niwahakikishie wananchi kwamba sina shaka na ushindi wa Chama cha Mapinduzi jambo la muhimu ni nyie mjitokeze kwa wingi kupiga kura oktoba 29,nimekuja hapa kumwombea kura za kishindo mgombea wetu wa urais na pia nimekuja kuwanadi mgombea wetu wa kiti cha ubunge pamoja na mgombea wa nafasi ya udiwani”,alisema.
'Mwamba' Haji Fundi Haji(kulia)akiomba kura za udiwani kwa wananchi wa kata ya Bondeni Manispaa ya moshi kwenye mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye kata hiyoAkizungumza
katika mkutano huo mgobmea wa kiti cha udiwani,Haji Fundi Haji alisema kata ya
Bondeni ambayo ni eneo la kibiashara kutokana na kuwa na masoko mawili
makubwa,Mbuyuni na manyema inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwamo suala la
miundombinu ya maji taka pamoja na ukosefu wa
taa za barabarani hali inayochangia uwepo wa matukio ya kiharifu.
Aliahidi
kujenga ofisi za serikali za mitaa kwa ajili ya kuwarahisisha huduma wananchi
wa kata hiyo endapo atachaguliwa kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi
katika Baraza la madiwani pamoja na kujenga ofisi itakayoshughulikia masuala ya
migogoro ya Ardhi kwa wananchi hao badala ya kutumia muda mwingi kufuata huduma
hiyo baraza la ardhi la wilaya.
Alipongeza
mfanikio ya serikali ya awamu ya sita chini ya Rais,Dkt.Samia Suluhu Hassan
katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake katika karibu zote kuanzia suala
la Afya,Elimu na miundombinu ya barabara ikiwamo mradi wa Treni ya mwendo kasi
(SGR)kutoka Dar es salaam hadi Dodoma mradi aliodai Rais aliukuta ukiwa aslimia
30 ya ujenzi.
Akimwombea
kura mgombea wa kiti cha Ubunge Jimbo la Moshi Mjini,Ibrahim Shayo maarufu kwa
jina la ‘Ibra Line’,Haji Fundi Haji alisema mgombea huyo amefanya mambo
mengi mazuri kwa wananchi wa Moshi mjini
kabla hajawaza kuwa mbunge na kuwaomba wampe kura nyingi katika uchanguzi mkuu
wa Rais,wabunge na madiwani hapo Oktoba 29 mwaka huu.
“Ndugu zangu wananchi wa kata ya Bondeni,siku zote wema hulipwa kwa wema,Ibra Line amefanya mengi kwa wananchi wa moshi mjini na nyie ni mashahidi,naombeni sana oktoba 29 twende tukalipe wema kwa ndugu yetu Ibra Line kwa kumpa kura nyingi za kishindo”,alisema.
Kwa upande
wake ,Irahim Shayo ambaye ni mmoja wa wafanyabiashara maarufu nchini katika
sekta ya usafrishaji na sekta ya mafuta alisema anajua changamoto za wananchi
wa kata ya Bondeni ambao wengi wao ni wafanyabiashara kama alivyo yeye.
“Ninajua
changamoto zenu kama wafanyabiashara wenzangu maana huko ndiko nimetoka,naomba
niwahakikishiek uwa kama mtanichagua kuwa mbunge wenu,hakuna mfanyabiashara
yoyote atakayeondolewa kwenye maeneo yenu”,alisema.
Alionyesha
pia kukerwa na mfumo wa majitaka kwa wananchi wa kata ya Bondeni na maeneo mengine
ya mji wa Moshi na kuahidi kushughulikia kero hiyo atakapochaguliwa kuwa mbunge
wa jimbo la Moshi mjini kwenye uchanguzi mkuu wa Rais,wabunge na madiwani
Oktoba 29 mwaka huu.
0 Comments