Afisa masoko wa kampuni ya kuzalisha mbolea za minjingu mkoani kilimanjaro,Abel Ngwagu(kulia)akitoa maelezo mafupi ya matumizi bora ya mbolea za minjingu kwa mkuu wa wilaya ya Rombo,Raymond Mwangwala (kushoto)kwenye tamasha la sita la kahawa(kahawa Festival)mjini moshi
MOSHI-KILIMANJARO
KAMPUNI ya kuzalisha mbolea ya Minjingu ya mkoani
Arusha imetumia Tamasha la sita la kuhamasisha unywaji wa kahawa nchini (Kahawa
Festival)lililofikia kilele chake jumapili octoba 5 mwaka huu mjini moshi kutoa
elimu ya matumizi bora ya mbolea za
minjingu kwa wakulima wa zao la kahawa .
Tamasha hilo
la sita la kuhamasisha unywaji wa kahawa limefanyika kwa siku tatu mjini moshi
katika kiwanda cha kukoboa kahawa cha Tanganyika Coffee Curing na kuzinduliwa
na mrajis wa vyama vya ushirika nchini,Dkt.Benson Ndiege.
Akizungumza
na vyombo vya habari katika Tamasha hilo,afusa masoko ya kampuni hiyo ya
Minjingu mkoani Kilimanjaro,Abel Ngwagu alisema kuwa,mbolea za minjingu ni
mbolea za asili.
Alisema mbolea
za minjingu zinatokana na mabaki ya
viumbe hai hivyo ni mbolea inayotunza unyevu pamoja na kutunza ardhi tofauti na
mbolea zingine hivyo mazao hayawezi
kunyauka.
“Tupo hapa
kutoa elimu juu ya matumizi bora na sahihi ya mbolea za minjingu kwa ajili ya
wakulima wa kahawa na wakulima wa mazao mengine kwani mbolea zetu ni za asili
zikitokana na mabaki ya viumbe hai”,alisema.
Kwa mujibu
wa afisa masoko huyo wa kampuni ya mbolea za minjingu ,mbolea hizo pia zipo
kwenye mfumo wa mbolea za ruzuki zikiuzwa kwa bei nafuu kuliko mbolea nyingine
ambako mfuko wenye ujazo wa kilogramu 50 wa mbolea ya kupandia NAFAKA DAAP PLUS
inauzwa sh,56,456.
Alisema
mbolea ya kukuzia yaani CAAN PLUS mfuko
wenye ujazo wa kilogram 50 inauzwa sh,53,414 na kutoa wito kwa wakulima wa
kahawa na mazao mengine kutumia mbolea za minjingu kwa ajili ya kupandia na
kukuzia.
Kwa faida ya wakulima wa zao la kahawa nchini mbolea aina ya COFFEE PLUS NPK 20:10:15 ambayo ni mbolea ya kuongeza uwezo wa mibuni ina viburudisho vya aina tano.
Abel Ngwagu,afisa masoko kampuni ya kuzalisha mbolea za minjingu mkoani Kilimanjaro akiwa kilele cha Tamasha la sita la Kahawa(Kahawa Festival)mjini moshi
Akihitimisha
kilele hicho cha Kahawa Festival,Mkuu wa wilaya ya Rombo,Mwalimu Raymond Mwangwala kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Nurdin Babu, aliwataka wakulima wa zao la kahawa na wananchi kwa ujumla kujivunia vitu vya
ndani.
Alisema ni
wajibu wa kila mtanzania kuwa balozi wa kuhamasisha unywaji wa kahawa na
kuongeza kuwa kama soko la ndani la kahwa litaimarika vijana wengi watapata
ajira.
“Tujivunie
vitu vyetu vya ndani ili hata bei ya kahawa kwenye soko la dunia likiyumba tusitetereka
lakini pamoja na kwamba kahawa ni kinywaji muhimu na ni cha pili duniani
ukiondoa maji bado soko la ndani linachngamoto”,alisema.
Aliwataka watanzania kupuuza propaganda zinazoenezwa na watu kwamba kahawa ina madhara mwilini na kueleza kuwa kahawa inazofaida nyingi mwilini ikiwamo kuchangamsha mwili pamoja na kuondoa msongo wa mawazo.



0 Comments