WAENDESHA
Bodaboda na Bajaj mkoani Kilimanjaro wamekutana na kuzungumzia vurugu
zilizotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu oktoba 29 mwaka huu
zilizosababisha uharibifu wa mali pamoja na vifo na kutoa neno.
Katika mkutano
wao wa siku moja kwenye ukumbi wa mikutano makao makuu ya polisi usalama
barabarani mkoa wa Kilimanjaro,wamesema waathirika wakubwa wa uvunjifu wa Amani
ni madereva wa Bodaboda na Bajaj na kuiambia dunia kuwa hawahusiki na vurugu
hizo ambazo ziliwaathiri kwa kiwango kikubwa.
Bahati Nyakiraria
mwenyekiti wa Bodaboda na Bajaj mkoa wa Kilimanjaro amesema tukio hilo
liliwaathiri kiuchumina kiafya na kwamba waliofanya vurugu hizo kwa kutumia Bajaj na Bodaboda si wao bali ni wahuni waliotumia vyombo hivyo na kujificha
kwenye mwamvuli wa Boda na Bajaj.
“Uvunjifu wa
Amani ukitokea wa kwanza kuathirika ni sisi kwa sababu tunabeba abiria,wengi
walioathrika ni abiria kwa sababu wanatumia usafiri wetu,wengine waliathirika
kiuchumi kiafya na wengine walipata mshtuko “,alisema.
Bahati amesema si kila anayeendesha boda boda au bajaj anafanya kazi kama yao,baadhi wanazitumia kwa malengo yasiyokusudiwa na kuwataka kila mmoja kuwa mlinzi wa Amani.
Amesema
jukumu la kuilinda na kutunza Amani ni jukumu la kila mtu na si kuwaachia
vyombo vya ulinzi na usalama wakiwamo polisi,na kuongeza amani ni jukumu la
watanzania wote.
Kutokana na
matukio hayo ya uvunjifu wa Amani serikali imeanza mchakato wa kuvisajili
vyombo hivyo vya moto ili kuwa na udhibiti kwa wale watakaotumia vyombo hivyo kutekeleza
uharifu ukiwamo uharifu wa kuoanga .
Akizungumzia
hilo Bahati amesema kuwa Bajaj na Bodaboda zitasajiliwa nakuingizwa kwenye
mfumo na mamlaka ya uhdibiti wa usafiri ardhini(LATRA) na wale watakaobainika
kufanya uharifu mfumo utawakataa.
Mfumo huo pia utakuwa mwarobaini wa matukio ya uporaji unaofanywa na waharifu ambao wamekuwa wakitumia bodaboda kupora watu katika maeneo mbali mbali nchini
Mwenyekiti wa Chama cha waendesha Bodaboda na Bajaj mkoa wa Kilimanjaro,Bahati Nyakiraria(kulia)akiwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Moshi mjini,Hamadi Bendera





0 Comments