TPC KUTUMIA BILIONI 130 UJENZI WA KONGANI YA VIWANDA

 

ENEO INAPOJENGWA KONGANI YA KIWANDA HUKO ARUSHA CHINI MOSHI VIJIIJINI HUU NI MKAKATI WA KIWANDA CHA SUKARI CHA TPC KATIKA KUPANUA WIGO WA UWEKEZAJI  

 

KIWANDA  cha sukari cha TPC kilichopo mkoani Kilimanjaro,kimeanza mkakati wa kuwekeza kwenye sekta ya viwanda itakayowezesha kupanua wigo na kuongeza thamani pamoja na kuongeza ajira baada ya kuanza ujenzi mkubwa wa kongani  ya viwanda ambako kiasi cha shilingi za kitanzania Bilioni 130 zitatumka. 

Mkakati huo wa TPC utafungua fursa za kiuchumi na inatarajiwa kutoa ajira 1,800 zikiwa ajira za kudumu za na muda mfupi . 

Kwa muda mrefu TPC imekuwa ikitumia  makapi ya miwa katika uzalishaji wa nishati ya umeme na kuokoa mamilioni ya fedha ambazo zingetumika kwa ajili ya kulipia Ankara za umeme kwa shirika la umeme Tanzania(Tanesco)kutokana na kuwa na kiwanda kikubwa cha kuzalisha nishati hiyo ya umeme. 

Mtendaji mkuu wa kiwanda hicho anayeshughulikia masuala ya utawala , Jaffari Ally amesema leo novemba 18,2025 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu, anatarajiwa kuweka jiwe la msingi kuashiria kuanza kwa ujenzi wa kongani hiyo  kitakachojengwa  Kata ya Arusha Chini, Wilaya ya Moshi. 

AFISA MTENDAJI MKUU WA KIWANDA CHA SUKARI CHA TPC ANAYESHUGHULIKIA UTAWALA,JAFFARI ALLY AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WAHABARI KUHUSIANA NA UJENZI WA KONGANI YA VIWANDA

Amesema ujenzi wa kiwanda hicho ukikamilika utazalisha  lita milioni 16.3 za Extra Neutral Alcohol maarufu Ethanol (ENA) na uzalishaji wa lita 400,000 za nishati Technical Alcohol inayotumika katika majiko poa kwa ajili ya kupikia majumbani.

Amesema kongani nyingine, itazalisha mbolea aina ya Potasium, ikakadiliwa kufikia  metriki tani 8,000 hii itatokana na kuchakatwa kwa  molasesi, baada ya kuzalishwa Ethanol. 

Kwa mujibu wa Jaffari,kiwanda hicho pia kitazalisha hewa ukaa lita 400,000 ambayo itakuwa mahususi kwa ajili ya matumizi ya viwandani pamoja na  uzalishaji wa mitambo ya kuzalisha umeme megawati sita zitakazouzwa kwa Tanesco. 

Amesma miradi hiyo inatarajia kukamilika mwezi Desemba mwaka 2026 nakuongeza kuwa miradi hiyo inakwenda pamoja na uwezo wa TPC ukusanyaji na  ulipaji wa  kodi pamoja na uboreshaji wa mazingira  mazingira lengo ni  kusaidiana na serikali katika juhudi zake za kuwa na nishati salama na safi.

 



Post a Comment

0 Comments