JENGO LA MAKAO MAKUU YA KNCU KAMA LINAVYOONEKANA KWA MBALI
KILIMANJARO
WANACHAMA wa Chama cha msingi cha
ushirika wa mazao(AMCOS)cha Kirima Boro kilichopo wilaya moshi mkoani
Kilimanjaro wamepaza sauti kuhusiana na mwenendo usioridhisha wa viongozi wa Bodi
ya uangalizi ya chama hicho kudaiwa kuuza mashamba yanayomilikiwa na chama
hicho kwa watu binafsi,wakiwamo wanasiasa,wafanyabiashara na watu wengine.
Kwamba Bodi hiyo ambayo imekuwa
madarakani kwa miaka mine kinyume na ilivyokuwa ya kuwa madarakani kwa siku 90 ,imekuwa
ikifanya yale ambayo hayakuwa makusudio ya uwepo wake.
Mheshimiwa mwenyekiti Bodi ya caretaker ya KIRIMA BORO AMCOS imefanya ufisadi mkubwa kuuza mali za Ushirika likiwemo ekari 7 za shamba la Sangiti. Nilishirikiana na Mwenyekiti wa Kijiji cha Boro Laurent Meja kwenda hadi TAKUKURU kutoa taarifa za Caretaker kukaa madarakani zaidi ya miaka 4 badala ya siku 90”
“Mwenyekiti, mali nyingine zilizouzwa bila ridhaa ya Mkutano Mkuu ni jembe la trekta na trailer,hakuna ukaguzi wa Mahesabu ya Ushirika ”
“ Ninayo taarifa kuwa Ukaguzi wa mwisho ni Mwaka 2021/2022 ambao umefichwa na Afisa Ushirika kwa sababu kuna taarifa ya ufisadi wa fedha nyingi zimeliwa na Wajumbe wa Bodi iliyokuwa chini ya .......(anataja jina)”
Huu ni ujumbe uliotumwa kwa kiongozi
mmoja wa chama cha mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro kutoka kwa mmoja wa wanachama wa chama hicho
akimuomba aingilie kati kuunusuru ushirika huo ili viongozi hao wasiendelee kuuza
mali za ushirika.
Oparesheni hiyo ilivikumba vyama
vikuu vya KNCU(Kilimanjaro),SHIRECU(Shinyanga),NYANZA(Mwanza) na maeneo mengine
ambako tume ya uchunguzi iliyoundwa na ofisi ya waziri mkuu wakati huo
ilifichua ufisadi mkubwa wa mali za wanaushirka.
Mkoani Kilimajaro ripoti ya ukaguzi
ikafichua mauzo tata ya shamba kubwa la
kahawa la Gararagua lililopo Wilaya ya Siha mali ya Chama Kikuu
cha Ushirika Mkoa wa Kilimanjaro (KNCU) ambako tume ilibaini liliuzwa chini ya thamani halisi ya bei ya soko, pamoja
na kutokujulikana zilipo ekari 2,000.
Shamba hilo liliuzwa mwaka 2017 na KNCU kwa dola za Marekanai
milioni 4.2 sawa na Sh bilioni 9.24,(kwa wakti huo) ikiwa ni mkakati wa chama
hicho kujinasua na madeni makubwa likiwamo deni la Sh bilioni 5.2 ambalo
chama hicho kilikuwa kinadaiwa na Benki ya CRDB.
Liliuzwa kwa Kampuni ya Tanbreed/Africado baada ya chama hicho
kuvunja mkataba na mwekezaji aliyekuwa akiendesha shamba hilo Kampuni ya Ocean
Link Shipping Services Limited na kukubali kumlipa fidia ya Sh bilioni 2.9
malipo ambayo yanadaiwa kugubikwa na utata pia.
KNCU ilivunja mkataba na mwekezaji huyo uliokuwa wa miaka 30 na
ambao ungefikia ukomo mwaka 2030, hivyo mwekezaji huyo alilipwa fidia hiyo ya
miaka 16 iliyobaki kulingana na mkataba wake kama angeendelea na uwekezaji.
Hata hivyo ripoti ya ukaguzi uliofanywa na Mkaguzi wa Ushirika
Mkoa wa Kilimanjaro ilibaini madudu mengi kwenye mchakato mzima wa kuuzwa kwa
shamba hilo ambalo kwa mujibu wa ripoti hiyo lilikuwa na ukubwa wa ekari 5,414
mwaka 1980.
Madudu hayo ndiyo yakaisukuma serikali kupitia kwa Waziri Mkuu
Kassim Majaliwa(wakati huo) kuunda timu ya kuchunguza uuzwaji wa shamba hilo na
matokeo ya uchunguzi huo ‘yakawasukuma’ ndani waliokuwa viongozi wa Bodi ya
KNCU.
Mwenyekiti wa bodi hiyo na makamu wake pamoja na aliyekuwa Meneja
wa KNCU, Honest Temba wakafunguliwa mashitaka ya uhujumu uchumi kwenye Mahakama
ya Hakimu Mkazi Moshi wakidaiwa kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia
KNCU hasara ya Sh bilioni 2.9.
Mbali na hao, walikuwemo pia viongozi wa Kiwanda cha Kukoboa Kahawa cha
Tanganyika Coffee Curing (TCCCo), Maynard Swai, aliyekuwa mwenyekiti wa
bodi na Andrew Kleruu aliyekuwa meneja wa kiwanda hicho nao walifikishwa
mahakamani wakidaiwa kutumia madaraka yao vibaya.kwa kununua mtambo wa kukoboa kahawa kutoka Kampuni ya Brazafric
ya Brazil bila kufuata taratibu na kuisababishia TCCCo hasara ya Sh bilioni
1.67.
Nimerejea ripoti hii ili jamii ijue kuwa mali hizi za ushirika si vihamba kwamba walioko madarakani wanagawa kama wanagawia familia zao(vihamba)na nimuombe mrajis wetu Dkt.Benson Ndiege asikubali mali za ushirika kuuzwa kama mali za ukoo.
Kwa wanaomfahamu Dkt.Ndiege ni mtu wa msimamo,ni kiongozi
asiyeweza kufumbia macho ufisadi wa mali za ushirika,ni mtu ukimwamsha usiku anawaza
ushirika,ukisema nae anawaza ushirika ni jukumu letu kumuunga mkono ili
kukomesha ufisafi wa aina hii
HAWA NI WANANCHI WA KIRIMA BORO MOSHI VIJIJINI WALIPOFIKA MJINI MOSHI KUPAZA SAUTI KUTAKA UUZWAJI WA SHAMBA LA USHIRIKA KIRIMA BORO AMCOS UKOMESHWE


0 Comments