SHAMBA LA SANGITI NI LA WAKULIMA?

  

Kuna sintofahamu ya nani hasa anamiliki shamba la Sangiti huko Kibosho baada ya kuibuka watu wanaodai shamba hilo si mali ya ushirika bali ni mali ya wakulima mmoja mmoja hivyo wanayo haki ya kuuza kama vihamba.

Shamba hilo lilikua linamilikiwa na raia wa kigeni na lilinunuliwa kupitia vyama viwili mwaka 1967 baada ya raia huyo wa kuwa na deni benki ,wakulima walikatwa fedha za mauzo ya kahawa hadi pesa ikatoshea.

Kwa faida ya wasomaji wetu,machi 21 mwaka 1967 vyama viwili vya msingi vya ushirika vya Kimasio na Kirima Boro viliandika barua ya kuomba kununua shamba lililokuwa likimiliwa na raia mmoja wa kigeni Tsoucas baada ya kubaini kuwa shamba hilo haliendelezwi .

“Vyama viwili vilivyotajwa hapo juu vinayo heshima kubwa kununua shamba hilo kwa manufaa ya watu wote,baada ya uchunguzi mwingi kwa wahusikao na shamba hilo ilionekana kuwa liko chini ya ulinzi wa manager wa Standard Bank”,inasema barua hiyo na kuongeza.

“Baada ya kumwona manager wa Bank alitoa dokezo kuwa shamba hilo ni ekari 450 na ni jumla ya sh,600,000,kwa kifupi,shamba hilo halina mastawisho yeyote bali kuna vyumba viwili tu(2),zaidi  ya  hapo tulikwisha julishwa kuwa alikuwa na deni la Bank jumla ya sh,15,000”.

Kuambatana na kima hicho cha sh,600,000,tunakuomba shamba hilo lichukuliwe kama bei hiyo ni ya halali,tunatumai kuwa ombi letu hili litafikiriwa kwa makini”,imehitimisha barua hiyo ambayo nakala yake timu yetu ya uchunguzi inayo .

Katika mahojiano ya hivi karibuni baadhi ya wananchi wanaoishi kirima wanasema wanaohusika na shamba hilo ni wale tu ambao walikubali kukatwa fedha zao za mauzo ya kahawa na si wananchi wote waliokatwa fedha kununua shamba hilo,

Wanajenga hoja kuwa wanaouza mashamba hayo kwa watu ndiyo wenye sauti ya kuzungumzia uuzwaji wa mashamba hayo na si kila mtu.

Hatua hii inakuja siku chache baada ya baadhi ya wanachama wa chama cha msingi cha ushirika cha Kirima Boro Amcos kupaza sauti kwa kuzitaka mamlaka za uchunguzi kuchunguza uuzwaji wa shamba hilo unaodaiwa kufanywa na Bodi ya usimamizi ya chama hicho.

Hali hiyo ilipelekea Tume ya maendeleo ya ushirika kupitia mrajis wa Ushirika nchini kutuma timu ya uchunguzi kuchunguza madai hayo.

Inaelezwa kuwa wakulima walikuwa wakikatwa senti saba  kwa kila ratiri ya kahawa waliyokuwa wakiuza chamani .

“Kila mtu anayomamlaka juu ya ardhi yake na hao wanaolalamika kwamba ardhi inauzwa si wanufaika wa hayo mashamba kwani hawakuwahi kukatwa fedha zao kwenye kahawa kununua mashamba hayo”

“Kuhusu mali zinazodaiwa kuuzwa tuhuma hizi zi za kweli kwani hiyo trekta na jembe vyote vipo na unaweza ukaenda chamani ukapiga picha”,anasema mmoja wa viongozi wa Bodi ya usimamizi.

Shamba hilo ambalo lilikuwa na ukubwa wa ekari 450 lilimegwa kwa ajili ya upanuzi wa Taasisi zikiwamo shule,makanisa,misikiti,kituo cha polisi na zanahati na kubakia ekari 142.

Baadae Kaskazini yenye vijiji vinne ,Kirima Juu,Maua,Otaruni na Singa na kusini yeney vijiji viwili ambavyo ni Kirima kati na Boro waliamua kugawa nusu kwa nusu kwa maana ya ekari 71 kila upande .

Kuhusu madai ya ujenzi wa ukumbi unaoendelea kujengwa chamani hapo ,viongozi hao wanasema taratibu zote zilizifuatwa na kupata baraka za wanachama .

Uongozi kwa kushirikiana na kamati ya shamba ili kutoa ekari 2 na nusu kwa mabadirishano ikiwa ni mkakati wa kupata pesa kufanikisha ujenzi huo.

Mwenyekiti wa Bodi hiyo Hashim Komu anasema suala hilo lilipelekwa kwa wanachama ambao waliridhia na juni 20 waka jana mkutano wa wananchama ulielekeza ifanyike tathimini ya gahraza za ujenzi wa ukumbi huo.

Anasema Mei 29 mwaka huu taarifa ya tathimini iliwasilishwa kwenye mkutano wa wanachama  na kupewa taarifa ya matokeo ya tathimini hiyo na kuridhia ujenzi uanze mara moja 

Kuhusu ukaguzi wa hesabu za chama,uongozi huo unasema kila msimu shirika la ukaguzi wa hesabu za vyama vya ushirika la CAOSCO kila msimu limekuwa likikagua hesabu za chama hicho kwamba taarifa za ukaguzi zipo .


Post a Comment

0 Comments