KUMEKUCHA KIRIMA BORO AMCOS,MRAJIS AIFUTILIA MBALI BODI YA UANGALIZI,NI BAADA YA KUHUSISHWA NA UUZAJI WA ARDHI YA USHIRIKA KAMA VIHAMBA

 OFISI YA CHAMA CHA MSINGI CHA KIRIMA BORO AMCOS

TUME  ya maendeleo ya Ushirika nchini kuptia ofisi ya Mrajis wa vyama vya ushirika imeifutilia mbali Bodi ya uangalizi ya  Chama cha ushirika cha Kirima Boro Amcos baada ya kutuhumiwa kujihusisha ya uuzaji wa sehemu ya shamba la Sangiti ambalo ni mali ya ushirika.

Uamuzi huo ambao ulikuwa unasubiliwa kwa hamu na wanachama wa chama hicho umekuja siku chache baada ya kuwepo na kelele nyingi kutoka kwa wananchama hao wakilalamikia kitendo hicho.

Baada ya kuifutulia mbali Bodi hiyo,Mrajis ametangaza kalenda ya uchaguzi wa Bodi mpya unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi huu huku akizuia viongozi waliokuwa kwenye Bodi hiyo kuwa sehemu ya watakaochukua fomu.

Uamuzi huo umefanywa hivi karibuni katika mkutano mkuu maalumu ulioitishwa na Mrajis mwenyewe na tayari baadhi ya wanachama wameanza kuchukua fomu za kugombea nafasi za ujumbe wa Bodi mpya.

Bodi huyo ilikuwa chini ya mwenyekiti wake Hashim Michael Komu ambako wajumbe ni Alberith Joseph Mushi,Abass Hatibu Kalanga,Aloyce August Kimaro na Mathew Ngowi.

Kabla ya uamuzi huo kufikiwa,mrajis alituma timu ya uchunguzi kuchunguza malalamiko ya wanachama hao ambao wanadai viongozi hao pia wameuza baadhi ya mali za ushirika ikiwamo trekta na jembe lake japo madai hayo yamekanushwa na viongozi hao



 

Kwa faida ya wasomaji wetu,tunakueletea taarifa yetu ya awali ambayo tuliichapisha hapa na namna shamba hilo lilivyopatikana kutoka kwa raia mmoja wa kigeni aliyekuwa akilitumia ambaye alishindwa kuliendeleza kutokana na kuzongwa na madeni yaliyotokana na mkopo wa Benki 



NANI ANAUZA MASHAMBA  YA CHAMA CHA USHIRIKA CHA KIRIMA BORO AMCOS KAMA VIHAMBA ?

 

WANACHAMA  wa Chama cha msingi cha ushirika wa mazao cha Kirima Boro Amcos kilichopo wilaya ya moshi Vijijini,wamepaza sauti kwa mamlaka za uchunguzi kupiga kambi kwenye ofisi za chama hicho na kufanya uchuguzi juu ya madai ya viongozi wa muda wa chama hicho kudaiwa kuuza mashamba ya chama hicho kama ardhi ya ukoo maarufu kama vihamba kwa lugha ya kabila la Kichagga.

Wanadai kuwa viongozi hao wamewauzia ardhi ya chama hicho watu mbalimbali wakiwamo wanasiasa,wafanyabiashara wakubwa na watumishi wa umma jambo ambalo wanadai haliendani na sera ya serikali katika mkakati wa kuendeleza ushirika nchini.

Timu yetu ya uchunguzi iliyopiga kambi kwenye ushirika huo imeibua mengi ambayo bado tunayafanyia uchunguzi ikiwamo majina ya waliouziwa ardhi hiyo Pamoja na kuwatafuta mmoja baada ya mwingine ili kupata kauli zao juu ya kuuziwa ardhi ya wanaushrika.

Kwa faida ya wasomaji wetu,machi 21 mwaka 1967 vyama viwili vya msingi vya ushirika vya Kimasio na Kirima Boro viliandika barua ya kuomba kununua shamba lililokuwa likimiliwa na raia mmoja wa kigeni Tsoucas baada ya kubaini kuwa shamba hilo haliendelezwi .

“Vyama viwili vilivyotajwa hapo juu vinayo heshima kubwa kununua shamba hilo kwa manufaa ya watu wote,baada ya uchunguzi mwingi kwa wahusikao na shamba hilo ilionekana kuwa liko chini ya ulinzi wa manager wa Standard Bank”,inasema barua hiyo na kuongeza.

“Baada ya kumwona manager wa Bank alitoa dokezo kuwa shamba hilo ni ekari 450 na ni jumla ya sh,600,000,kwa kifupi,shamba hilo halina mastawisho yeyote bali kuna vyumba viwili tu(2),zaidi  ya  hapo tulikwisha julishwa kuwa alikuwa na deni la Bank jumla ya sh,15,000”.

Kuambatana na kima hicho cha sh,600,000,tunakuomba shamba hilo lichukuliwe kama bei hiyo ni ya halali,tunatumai kuwa ombi letu hili litafikiriwa kwa makini”,imehitimisha barua hiyo ambayo nakala yake timu yetu ya uchunguzi inayo .

Kulingana na uchunguzi wetu,Desemba 14 mwaka 2023 mwenyekiti wa Kijiji cha Boro,Laurent Mushi kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho alimwandikia barua mkuu wa wilaya ya Moshi akilalamikia mwenendo wa uongozi huo kuuza ardhi ya shamba la ushirika kama vihamba akimuomba  kuingilia kati lalamiko hilo na kumuomba azuie mpango wa kugawa ardhi ya ushirika.

“Mh.Mkuu wa wilaya baadhi ya wanakijiji wenye nia njema ya kudumisha amani wanakuomba uingilie kati lalamiko hili na kuzuia mpango wa kugawa ardhi ya Ushirika inayosimamiwa na Chama cha ushirika cha msingi cha Kirima Boro”.

Uratibu wa kumilikisha vipande vidogo vidogo vya ardhi usimame na badala yake eneo libaki kwa ajili ya Taasisi muhimu kwa umma mfano;Kituo cha Afya,Kituo cha Polsi Chuo cha ufundi n.k”.

“Wanakijiji wamenieleza kuwa hofu yao ni kwamba mpango huu ukifanyika bila kuweka utaratibu wa kisheria wa kumilikisha ardhi ambayo ni mali ya Ushirika,viashiria vya ugomvi vinaweza kutokea katika shamba na kusababisha uvunjifu wa amani siyo tu kwa wanachama wa chama cha Ushirika cha msingi bali pia kwa wakulima ambao baba zao au mama zao ndio waliochangia fedha za kununua ardhi hiyo mwaka 1967 kutoka kwa wamiliki wa kigeni na wamekuwa wakijiuliza maswali yafuatayo…….”

 

Post a Comment

0 Comments